Wasilisha na Lipa
PAYE ni nini?
PAYE ni mbinu ya kukusanya ushuru kutoka kwa watu binafsi, Mkazi na mkazi wa kigeni, katika ajira yenye faida.
Faida au Mapato ni pamoja na mishahara, malipo ya likizo, malipo ya ugonjwa, malipo badala ya likizo, ada, posho, bahashishi, Takrima, au riziki, usafiri, burudani au marupurupu mengine inayopokelewa kuhusiana na ajira au huduma zinazotolewa.
Nani anapaswa kusajiliwa kwa mfumo wa PAYE?
Mtu yeyote anayelipa mishahara kwa mfanyakazi au wafanyikazi anapaswa kujisajili katika mfumo wa PAYE ambapo anahitajika
- Kukata kodi kwa malipo apatayo mfanyikazo au wafanyi kazi
- Kulipa kodi iliyokatwa kwa mamlaka ya KRA
Kama mwajiri unapaswa kukata PAYE kutoka kwa mshahara na malipo ya vibarua ya wafanyikazi wako kwa viwango viliwepo na kulipa sawa kwa KRA kabla ya tarehe 9 ya mwezi uliofuata.
PAYE inatozwa kwa watu wenye mapato ya ajira ya Kshs. 24,000 na zaidi kwa mwezi.
Faida zisizo za pesa zinazotozwa kodi
Mapato au Faida kutokana na ajira ambayo haijalipwa kwa fedha taslimu hutozwa kodi. Mapato au faida kama hizi
- Nufaiko la gari
- Nufaiko la nyumba
- Mikopo yenye riba ya chini kuliko kiwango cha soko kilichopo
- Matumizi ya kinyumbani mfano maji,umeme,usalama,matumizi ya simu na gharama za nyumbani zisizozidi kiwango ruhusiwa cha shilingi 3,000 kwa mwezi
- Mchango wa malipo ya uzeeni unaolipwa na mwajiri mwenye msamaha wa kodi kwa mpango ambao haujasajiliwa.
- Mchango wa malipo ya uzeeni unaolipwa na mwajiri kwa mpango ambao umesajiliwa au haujasajiliwa uliozidi kiwango ruhusiwa cha shilingi 20,000 au 240,00 kwa mwaka
Ni mapato gani ambayo hayatozwi mfumo wa PAYE?
- Milo inayotolewa na mwajiri hadi kiwango cha juu cha shilingi 4,000 kwa mwezi au shilingi 48,000 kwa mwaka.
- Nufaiko la Kulala nje kikazi la shilingi 2,000 kwa siku
- Kiasi ambacho ni marejesho tu ya gharama,k.m posho la kujikimu kwenye shughuli rasmi(per diems) au posho ya umbali wa safari haizingatiwi kwa malipo ya kodi
- Bima ya Matibabu unayolipiwa na mwajiri
- Kwa upande wa wakaazi wa kigeni ambao wako nchini Kenya kumtumikia mwajiri pekee, matumizi ya mapito kati ya Kenya na sehemu yoyote nje ya Kenya yanayogharamiwa na mwajiri.
- Mchango wa malipo ya uzeeni unaotolewa na mwajiri, anayetozwa kodi, kwa mpango ambao umesajiliwa au haujasajiliwa uliopo kwenye kiwango ruhusiwa cha shilingi 20,000 kwa mwezi au 240,000 kwa mwaka
- Mchango wa malipo ya uzeeni unaolipwa na mwajiri mwenye msamaha wa kodi kwa mpango ambao umejasajiliwa uliopo kwenye kiwango ruhusiwa cha shilingi 20,000 kwa mwezi au 240,000 kwa mwaka
- Pesa inayolipwa na mwajiri kwa mpango wa mafao ya kustaafu uliosajiliwa chini ya kikomo cha Kshs. 240,000 kwa mwaka hazitozwi kodi. Hata hivyo msamaha huo haupatikani kwa watu binafsi ambao tayari wanafurahia kukatwa kwa michango ya mpango wa mafao ya kustaafu uliosajiliwa.
- Ada ya elimu ya wategemezi wa mfanyakazi au jamaa inayolipwa kutokana na mapato ambayo tayari yametozwa kodi mikononi mwa mwajiri;
Mapunguzo yanayoruhusiwa
Hivi ni viwango vinavyotolewa kwa malipo ya mfanyikazi ili kufikia kiasi kitakachotozwa kodi.
Kukatwa kwa Riba ya Rehani
Riba inayolipwa kwa kiwango kilichokopwa kutoka kwa taasisi tano za kwanza za kifedha zilizoainishwa katika ratiba ya nne ya Sheria ya Kodi ya Mapato, aidha kwa ununuzi au uboreshaji wa majengo yanayokaliwa kwa madhumuni ya makazi hukatwa dhidi ya mapato ya ajira, hadi kiwango cha juu cha shilingi 300,000 kwa mwaka.
Michango ya malipo ya uzeeni anayolipa mfanyikazi kwa hazina ya malipo ya uzeeni iliyosajiliwa.
Mapunguzo yanayoruhusiwa ni ya kiwango kisichozidi shilingi 20,000 kwa mwezi.
Unafuu wa Kodi
Unafuu wa Kibinafsi
Unafuu wa Kibinafsi unapewa kwa wakaazi.
Inakusaidia kusahilisha mzigo wa kodi kwa walipa kodi.
Kwa sasa ni shilingi 2,400 kwa mwezi au Shilingi 28,800 kwa mwaka.
Unafuu Wa Kibima
unafuu wa kibima hupewa kwa mfanyakazi ambaye amelipa malipo ya bima ya maisha au sera za afya au elimu kwa ajili yake mwenyewe, mke au mtoto wake.
Unafuu hupewa kwa Asilimia 15% ya malipo yanayolipwa hadi kiwango kizichozidi Shilingi 60,000 kwa mwaka.
Kwa elimu na afya, sera inapaswa kuwa na Muda wa ukomavu wa angalau miaka 10.
Kuanzia tarehe 1 Januari 2022, michango kwa Hazina ya Kitaifa ya Bima ya Afya (NHIF) inastahili unafuu wa bima.
PAYE Inakokotolewaje?
PAYE inakokotolewa hivi:
Asilimia na viwango vya ushuru vya mtu binafsi
Asilimia zifuatazo za kodi zitatumika kwa mapato ya ajira ya kibinafsi kuanzia tarehe 1 Januari 2021. Marejesho ya kwanza chini ya kiwango kipya yatalipwa kufikia tarehe 9 Februari 2021.
Viwango vya ushuru | Mwaka | Kila mwezi | Asilimia |
Cha Kwanza | Shilingi. 288,000 | Shilingi. 24,000 | 10% |
Cha Pili | Shilingi.100,000 | Shilingi. 8,333 | 25% |
Juu ya mapato yote zaidi ya | Shilingi. 388,000 | Shilingi. 32,332 | 30% |
Unafuu wa kibinafsi wa Shilingi. 28,800 kwa mwaka (Shilingi. 2,400 kwa mwezi) |
Kwa malipoo ya uzeeni viwangoi vipya ni vifuatazo
Viwango vya Ushuru wa Malipo ya Uzeeni | Asilimia wa Ushuru kwa Mwaka |
Viwango vyovyote vinavyozidi msamaha kodi | |
Kwa shilingi 400,000 ya kwanza | 10% |
Kwa shilingi 400,000 inayofuata | 15% |
Kwa shilingi 400,000 inayofuata | 20% |
Kwa shilingi 400,000 inayofuata | 25% |
kwa kiwango chochote kinachozidi shilingi 1,600,000 | 30% |
Kwa mfano:
Viwango kuanza Kutumika Tarehe 01.01.2021 |
|
mapato ya Jumla kutokana na ajira |
Shilingi 115,000 |
Toa mapunguzo yanayoruhusiwa |
|
Riba ya Rehani |
Shilingi 15000 |
Mchango wa Malipo ya Uzeeni na Mfanyakazi |
Shilingi 5,000 |
Malipo yanayostahili kukatwa kodi |
Shilingi 95,000 |
Ya kwanza |
24,000*10% = Shilingi 2,400 |
Inayofuata |
8,333*25% = Shilingi 2,083.25 |
Inayofuata
|
|
Juu ya |
(95,000-32333) 62,667*30%=18800 |
Jumla ya kodi = 2400+2083.25+18800 = 23283,25 |
|
Toa |
|
Unafuu wa kibinafsi ya kila mwezi |
2400 |
Unafuu Wa Kibima |
0 |
Kodi inayostahili kulipwa |
20,883.25 |
Unaweza pia kutumia Kikokotoo wa PAYE ili kubaini Kodi inayostahili kulipwa.
Nitajazaje PAYE
Marejesho ya PAYE yanawasilishwa mtandaoni kupitia iTax
iwapo huna PAYE ya kuwasilisha inatakiwa kujaza marejesho hakuna(Nil Returns)
Nitalipaje PAYE
Baada ya kuwasilisha rejesho mtandaoni kupitia iTax, toa hati ya malipo na uwasilishe katika benki yoyote iliyoidhinishwa ya KRA ili ulipe kodi inayodaiwa.
Unaweza pia Kulipa kupitia Mpesa.
Tumia Nambari Ya Malipo (PayBill) 572572.
Nambari ya Akaunti ni nambari ya Usajili wa Malipo iliyonukuliwa kwenye kona ya juu kulia ya hati ya malipo inayozalishwa.
Ni nini adhabu ya kuchelewa kujaza na kulipa?
Date: Rejesha inapaswa kuwasilishwa na kodi ilipwe mnamo au kabla ya tarehe 9 ya mwezi unaofuata.
Adhabu kwa kuchelewa kuwasilisha kodi: Utalipa iliyo juu kati ya 25% ya ushuru unayodaiwa au shilingi 10,000
Adhabu kwa kuchelewa kulipa kodi: 5% ya ushuru unaodaiwa na malipo ya marehemu ya 1% kwa mwezi kwenye ushuru ambao haujalipwa hadi ushuru ulipwe kamili.
Maswala Ibuka
- Tofauti kati ya mtajiri na mshauri
- Kutojumuishwa kwa faida zinazotuzwa kodi
Kujaza PAYE
Je, mapato yako yanatokana na ajira pekee?
Tazama video ya jinsi ya kujaza kodi ya mapato yatokanayo na Ajira Pekee